Raila: Mwindaji anayejua kujitafutia windo chakani

Rubrique

KIONGOZI wa Azimio la Umoja Raila Odinga, ameibukia kuwa mwanasiasa anayejua kujijenga upya na kutorokea baridi ya kisiasa, hata wakati anaposhindwa kwenye chaguzi za urais.

Tangu alipowania urais kwa mara ya kwanza mnamo 1997, Bw Odinga amebuni mbinu ya kutumia ujanja wa kisiasa kuhakikisha “anafaidika” pia kutoka kwa serikali inayochukua uongozi.

Kulingana na wadadisi wa siasa, hilo limedhihirishwa na juhudi zinazoendeshwa na Rais William Ruto kumpigia debe Bw Odinga kupata uungwaji mkono wa mataifa mengine barani Afrika, kwenye nia yake ya kuwania uenyekiti katika Tume ya Umoja wa Afrika (AUC).

Kinaya ni kwamba, licha ya Rais Ruto kuendesha juhudi hizo, wawili hao walikuwa washindani wakali kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9, 2022, kiasi kwamba walikuwa wakielekezeana cheche kali za maneno wakati wa kampeni.

Baada ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kumtangaza Dkt Ruto kama mshindi wa uchaguzi wa urais, Bw Odinga na washirika wake katika Azimio waliapa kutomtambua Dkt Ruto kama Rais.

Hata hivyo, wawili hao baadaye waliondoa tofauti zao, duru zikieleza tayari kuna handisheki fiche baina ya vigogo hao wawili.

Wadadisi wanasema Rais Ruto na Bw Odinga walibuni handisheki hiyo kwenye kikao cha faragha kilichofanyika Oktoba mwaka uliopita jijini Mombasa.

Kikao hicho kilimshirikisha rais wa zamani wa Nigeria, Bw Olusegun Obasanjo.

“Hatua ya Rais Ruto kuanza kumfanyia kampeni Bw Odinga kuwania nafasi ya mwenyekiti katika AUC, inamsawiri Bw Odinga kama mwanasiasa mjanja mwenye uwezo wa kujiunda upya, kwa kuhakikisha kuwa pia amefaidika kutoka wa serikali iliyopo mamlakani,” asema Bw Micah Mutai, ambaye ni mchanganuzi wa siasa.

Matukio mengine yanayotajwa kumsawiri Bw Odinga kama mwanasiasa mjanja ni hatua yake kubuni ushirikiano na Rais Mstaafu (marehemu) Daniel Moi, ambapo aliteuliwa kama Waziri wa Kawi mnamo 1998.

Wakati huo, Bw Odinga alibuni ushirikiano wa kisasa na Bw Moi, ambapo wawili hao waliunganisha vyama vya Kanu na National Development Party (NDP)—chake Bw Odinga—na kubuni New-Kanu.

Baada ya Bw Odinga kushindwa na Rais Mstaafu (marehemu) Mwai Kibaki kwenye uchaguzi wa urais wenye ushindani mkali wa 2007, alikataa kutambua matokeo hayo.

Msimamo mkali wa Bw Odinga ndio ulimfanya kuteuliwa kama Waziri Mkuu kati ya 2008 na 2013. Washirika wake wa karibu pia walifaidika kutokana na nyadhifa za mawaziri kwenye Serikali ya Muungano wa Kitaifa.

Baada ya uchaguzi mkuu wa 2017, Bw Odinga alianzisha maandamano makali dhidi ya Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta, huku akikataa kutambua ushindi wake.

Kama njia ya kutuliza hali, ilimlazimu Bw Kenyatta kubuni handisheki na Bw Odinga.

Wadadisi wanasema kuwa ikiwa Bw Odinga atashinda uenyekiti katika AUC, basi hilo litamsawiri kama mwanasiasa mjanja, anayejua “kuchumia kivulini”.

Connexion utilisateur

Commentaires récents

  • Municipales 2026 en l'île aux fleurs fanées : les mots qu'on n'a pas entendus

    24%...

    Albè

    29/03/2026 - 15:16

    Le bâti (maisons, immeubles, routes etc...) ne couvre que 24% du territoire martiniquais. Lire la suite

  • Municipales 2026 en l'île aux fleurs fanées : les mots qu'on n'a pas entendus

    Superbe article !! Bande d'ordures ,va !!!!!....

    yug

    29/03/2026 - 13:41

    Superbe article ,notamment EN CE QUI CONCERNE LES PLU ET LES TERRES AGRICOLES .Ceci constitue e Lire la suite

  • Maires issus de l'immigration : la fin du « blocage », selon un démographe

    AUTOUR DU POT

    Albè

    29/03/2026 - 06:35

    Vous tournez autour du pot comme une bourrique ivre parce que vous êtes coincé. Lire la suite

  • Maires issus de l'immigration : la fin du « blocage », selon un démographe

    De qui parlez-vous ?

    yug

    28/03/2026 - 22:21

    ...quand vous dites :"En effet, on a vu ce qu'ils ont fait des Juifs à Auschwitz et Dachau.." ? Lire la suite

  • Maires issus de l'immigration : la fin du « blocage », selon un démographe

    "R"

    Albè

    28/03/2026 - 20:22

    Bakayoko ne roule pas les "R" comme les Africains, espèce de conard que t'es ! Lire la suite