Kenya yachagua kikosi cha kuteka dunia mbio za nyika

MABINGWA mara 23 wa dunia Kenya wamechagua kikosi cha kudondosha mate kwa makala ya 45 ya Mbio za Nyika za Dunia zitakazofanyika jijini Belgrade, Serbia mnamo Machi 30, 2024.

Agnes Ngetich, Emmaculate Anyango na Lilian Kasait wanaokamata nafasi tatu za kwanza kwa muda bora duniani mwaka huu katika mbio za kilomita 10 za barabarani wa dakika 28:46, 28:57 na 29:32, mtawalia, wako katika kikosi cha taifa cha wakimbiaji 30 kilichochaguliwa katika uwanja wa Chuo cha Mafunzo cha Magereza mjini Ruiru, Kiambu, Jumamosi.

Beatrice Chebet na Ngetich waliozoa dhahabu na shaba mtawalia kwenye Mbio za Nyika za Dunia 2023 nchini Australia, bingwa wa 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Margaret Chelimo pamoja na mshindi wa mbio za nyika za majeshi Cintia Chepngeno wanakamilisha orodha ya washiriki sita watakaotimka kitengo cha 10km cha wanawake. Chepngeno alikosa kumaliza mbio nchini Australia kwa hivyo amepata fursa nzuri ya kujifariji.

Bingwa wa dunia 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Sebastian Sawe ataongoza kikosi cha 10km wanaume kilicho na mfalme wa mbio za nyika kitaifa 2022 Samuel Chebolei, bingwa wa dunia mara mbili mbio za nyika Geoffrey Kamworor pamoja na Gideon Rono, Benson Kiplagat na bingwa wa dunia kitengo cha chipukizi 2023 Ishmael Kipkurui.

“Nilikuwa na matumaini makubwa ya kutwaa tiketi. Mpango wangu wa kutoonekana na kuchomoka zikisalia mita 500 naona ulifanya kazi vizuri,” akasema Sawe anayelenga medali jijini Belgrade.

Reynold Cheruiyot aliyemaliza nyuma ya Kipkurui pamoja na washindi wa dhahabu ya mbio mseto Emmanuel Wanyonyi na Kyumbe Munguti, sawa na Diana Chepkemoi, Emmanuel Wanyonyi na Charles Rotich watapata fursa ya kuimarisha matokeo yao kutoka mwaka 2023.

Timu ya chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 ya Kenya inajumuisha Sheila Chebet, Deborah Chemutai, Nancy Cherop, Mercy Chepkemoi, Diana Cherotich na Diana Chepkemoi (wanawake kilomita sita) na Samuel Kibathi, Charles Rotich, Mathew Kipkoech, Jonah Erot, Shadrack Rono na Gideon Kipngetich (wanaume kilomita nane).

Cheruiyot, Wanyonyi, Munguti, Virginia Nyambura, Mercy Wanjiru na Purity Chepkirui watashiriki mbio mseto.

Connexion utilisateur

Commentaires récents

  • Sa bel ba zot sé Afritjen-an !

    @Lidé, c’est surtout Saint-Domingue...

    Frédéric C.

    24/01/2026 - 22:04

    ...(République Dominicaine) de Trujillo qui est connue pour avoir voulu "blanchifier" sa populati Lire la suite

  • SOUTIEN AU PEUPLE GROENDLANDAIS POUR SON INDEPENDANCE

    Réponse à @Lidé

    tim

    24/01/2026 - 19:05

    Je ne suis pas un "défenseur "de ce que tu appelles "la grande civilisation blanche "et je ne tie Lire la suite

  • SOUTIEN AU PEUPLE GROENDLANDAIS POUR SON INDEPENDANCE

    Tim-hitler :stop le mensonge

    @Lidé

    24/01/2026 - 13:59

    L'Occident n'a rien apporter à l'humanité. ( Si : le génocide)
    Lire la suite

  • SOUTIEN AU PEUPLE GROENDLANDAIS POUR SON INDEPENDANCE

    T'ES QU'UN PAUVRE NAZE !

    Albè

    24/01/2026 - 12:43

    Chauve, prostatique, sénile, au regard bilieux dont "la pensée" ne casse pas trois pattes à un ca Lire la suite

  • SOUTIEN AU PEUPLE GROENDLANDAIS POUR SON INDEPENDANCE

    .....

    tim

    24/01/2026 - 12:15

    N'essaye pas de lutter contre moi .Je suis plus fort que toi.

    Lire la suite